Imewekwa: 08 Jun, 2022
Mamlaka inawataarifu madereva wote wanaoendesha magari ya biashara kuwa, imeanza rasmi kupokea maombi ya kufanya mitihani ya kuthibitishwa. Kwa kuanzia, mitihani ya Uthibitishaji inafanyika katika ofisi za Makao Makuu ya LATRA, zilizopo mtaa wa Nkrumah Jijini Dar es Salaam Jumatatu hadi Ijumaa mara mbili (2) Asubuhi na Mchana kulingana na muda uliowekwa kwenye mfumo.