Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara ya Uchukuzi

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini

Piga Bure : 0800110019/0800110020
LATRA Logo

Kurejesha Ratiba za Mabasi Tisa Yanayoanza Safari Saa 9.00 Alfajiri
Imewekwa: 11 Aug, 2023

Mnamo tarehe 19 Juni, 2023 Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) ilisitisha ratiba ya mabasi ya Ally’s Star na Katarama Luxury kuanza safari saa tisa (9:00) alfajiri na saa kumi na moja (11:00) alfajiri na kupewa ratiba ya kuanza safari saa kumi na mbili (12:00) asubuhi. Hatua hiyo ilitokana na Mamlaka kupata  taarifa na kuthibitisha uwepo wa mabasi  ya kampuni hizo yanayokwenda mikoani kuchezea Mfumo wa Kufuatilia Mwenendo wa Mabasi (Vehicle Tracking System - VTS) hivyo kusababisha kusafiri kwa mwendo kasi  kwa lengo la kufanya mashindano ya kuwahi kufika kwenye vituo/stendi za mabasi.

Hivyo Mamlaka kwa kuzingatia jukumu lake la kukuza usalama katika sekta zinazodhibitiwa ikiwa ni pamoja na usalama wa watumiaji wa huduma haiwezi kuacha matendo haya hatari yenye kuhatarisha usalama wa abiria na mali zao bila kuchukua hatua stahiki.

Pakua taarifa kamili

Mrejesho

Mrejesho, Malalamiko au Wazo