Nyaraka zinazohitajika
a) Kadi ya usajili wa gari;
b) Hati ya bima iliyo hai;
c) Hati ya ukaguzi wa gari kutoka Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani pamoja na risiti yake ya malipo.
d) TALA (kwa maombi ya leseni ya huduma ya usafirishaji gari la kubeba watalii)
e) Leseni ya dereva kwa magari ya abiria
Hatua za Kufuata
a) Kupata linki ya mfumo, ingia kwenye tovuti ya Mamlaka www.latra.go.tz, fungua huduma mtandao kisha chagua RRIMS. (Unaweza pia kupata linki ya mfumo moja kwa moja kwa kuandika www.rrims.latra.go.tz )
b) Itafunguka linki ya mfumo wa RRIMS, kisha ingiza baruapepe na nywila yako kwenye sehemu husika,
c) Chagua neno lililoandikwa Maombi ya leseni, bonyeza maombi ya leseni magari ya abiria,
d) Chagua neno Ongeza gari,
e) Jaza na hifadhi taarifa zinazohitajika, ambatisha nakala za vielelezo vinavyohitajika kisha, wasilisha maombi hayo kwenye ofisi ya LATRA ulilochagua,
f) Maombi ya leseni yatashughulikiwa ndani ya saa ishirini na nne (24),
g) Msafirishaji utapata ankara ya malipo (Control number)
h) Utalipia kupitia ankara ya malipo (Control number)/namba ya kumbukumbu ya malipo kwa kutumia huduma za kifedha kwenye mitandao ya simu. (tigopesa, Mpesa,Airtel Money, Halopesa, T-pesa n.k) benki na mawakala wa benki (NMB, NBC, Azania, nk)
i) Baada ya malipo unaweza kuchapa leseni yako mtandaoni kupitia akaunti yako ya RRIMS.
Zingatia
Hatua za maombi ya leseni, zitafuatwa na waombaji wa leseni wanaohuisha leseni, kubadili njia/huduma/ratiba baada ya mwombaji wa leseni kuchagua huduma anayohitaji.
Uhai wa Leseni: Mwaka mmoja
Gharama za maombi ya leseni
i) Gharama ya kubadili taarifa za mmiliki ni TZS. 10,000/=
ii) Unapotuma maombi ya leseni gharama yake ni TZS. 30,000/=
iii) Ada ya nakala iliyozalishwa kwa mfumo wa kielektroniki ni TZS. 50,000/=
iv) Malipo ya ratiba ya safari kwa magari ya masafa marefu (yanayounganisha mkoa na mkoa au nchi na nchi) ni TZS. 50,000/=
v) Gharama ya Kitabu cha kumbukumbu za safari (Logbook) ni TZS. 50,000/=
vi) Gharama ya kibali cha dharura ni TZS. 50,000/=
vii) Gharama ya kuvuka mpaka ni TZS. 100,000/=
viii) Gharama ya cheti cha usajili wa kampuni ya usafirishaji TZS. 100,000/=
ix) Gharama ya kubadili njia ni 40% ya gharama ya leseni kwa mwaka
Gharama za leseni
a) Leseni za Mabasi ya Abiria (Shule/wanafunzi, taasisi/Wafanyakazi, Daladala, Mabasi ya Mikoani.)
i) Daraja la Kawaida na Daraja la Kati la Chini
- Gari linalobeba abiria 25 hadi 45 TZS. 250,000/=
- Gari linalobeba abiria 45 hadi 65 TZS. 300,000/=
- Gari linalobeba abiria zaidi ya 65 TZS. 350,000/=
- Gharama ya maombi ya leseni kwa mwaka ni TZS. 50,000/=
- Gharama ya kubadili njia ni 50% ya gharama ya leseni kwa mwaka
ii) Daraja la Kati la Juu
- Gari linalobeba abiria 45 hadi 65 TZS. 250,000/=
- Gari linalobeba abiria zaidi ya 65 TZS. 300,000/=
- Gharama ya maombi ya leseni kwa mwaka ni TZS. 50,000/=
iii) Daraja la kati la Kifahari
- Gari linalobeba abiria 45 hadi 65 TZS. 300,000/=
- Gari linalobeba abiria zaidi ya 65 TZS. 300,000/=
- Gharama ya maombi ya leseni kwa mwaka ni TZS. 50,000/=
- Gharama ya kubadili njia ni 50% ya gharama ya leseni kwa mwaka
iii) Magari ya Abiria
- Gari linalobeba abiria wasiozidi 15 TZS. 100,000/=
- Gari linalobeba abiria 15 hadi 25 TZS. 200,000/=
- Gari linalobeba abiria 25 hadi 45 TZS. 250,000/=
- Gari linalobeba abiria 45 hadi 65 TZS. 300,000/=
- Gari linalobeba abiria zaidi ya 65 TZS. 350,000/=
- Gharama ya maombi ya leseni kwa mwaka ni TZS. 50,000/=
- Gharama ya kubadili njia ni 50% ya gharama ya leseni kwa mwaka
iv) Magari ya Shule
- Gharama ya maombi ya leseni ni TZS. 10,000/=
- Gharama ya kubadili taarifa za umiliki ni TZS. 10,000/=
- Gari linalobeba abiria 15 ni TZS. 100,000/=
- Gari linalobeba abiria 16 hadi 25 ni TZS. 200,000/=
- Gari linalobeba abiria zaidi ya 25 TZS. 300,000/=
iv) Usafiri wa Mabasi Yaendayo Haraka (BRT)
- Gari linalobeba abiria 45 ni TZS. 500,000/=
- Gari linalobeba abiria 45 hadi 65 ni TZS. 800,000/=
- Gari linalobeba abiria zaidi ya 65 ni TZS. 1,000,000/=
b) Leseni za Magari ya Kubeba Watalii.
- Gharama ya maombi ya leseni ni TZS. 10,000/=
- Gharama ya kubadili taarifa za mmiliki ni TZS. 10,000/=
- Gari linalobeba abiria wa kitalii 8 ni TZS. 250,000/=
- Gari linalobeba abiria wa kitalii 9 hadi 15 ni TZS. 350,00/=
- Gari linalobeba abiria wa kitalii 16 hadi 25 ni TZS. 750,000/=
- Gari linalobeba abiria wa kitalii 26 hadi 35 ni TZS. 1,000,000/=
- Gari linalobeba abiria wa kitalii 36 hadi 45 ni TZS. 1,250,000/=
- Gari linalobeba abiria wa kitalii zaidi 45 ni TZS. 1,500,000/=
Zingatia
Malipo yote yafanyike kwa ankara ya malipo (Control number)/ namba ya kumbukumbu ya malipo iliyotolewa na Mamlaka.

