Awali ya yote, namshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema kwa kuendelea kutupa uhai, afya na kuibariki Serikali yetu ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi mahiri wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Pia nashukuru kwa heshima niliyopewa na LATRA ya kuwa mgeni Rasmi katika hafla hii ya kukabidhi Cheti cha Uwakala wa Kutoa Leseni za Usafirishaji kwa Chama cha Kuweka na Kukopa Ushirika cha Maafisa Usafirishaji wa Pikipiki mkoa wa Dar es salaam (MAUPIDA SACCOS LTD). Pia, nafahamu kuwa Aprili 04, 2025 Mhe. Edward Mpogolo, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, alikabidhi cheti cha ushirika kwa chama hiki cha MAUPIDA SACCOS LTD kufuatia jitihada nyingi alizozifanya za kushirikiana na wadau wengine kuhakikisha kuwa Ushirika huu unaanzishwa.