Imewekwa: 14 Dec, 2022
Kabla ya kuongea zaidi kuhusu mkutano huu wa leo, naomba niseme yafuatayo kwa ufupi kabisa, Sote ni mashahidi kuwa Serikali ya awamu ya Sita, chini ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanya juhudi za kipekee kuhakikisha inakuza sekta binafsi kwa kuhakikisha sekta binafsi ndio inakuwa chachu ya kusukuma uchumi na chanzo cha mapato ya serikali kupitia kodi na kuongeza ajira kwa vijana hasa kwenye huduma za usafiri aridhini ikihusisha magari ya kukodi na huduma za usafiri wa mijini kwa kutumia mabasi na pikipiki za miguu miwili na mitatu.