Imewekwa: 27 Jul, 2022
Mkurugenzi Mkuu wa LATRA CPA Habibu Suluo, ametoa salamu za pole kwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Brigedia Jenerali Marco Gaguti kufuatia vifo vya watu 12 na majeruhi 17 vilivyotokana na ajali mbaya iliyotokea leo tarehe 26 Julai, 2022 eneo lenye mteremko la Mji Mwema, kata ya Magengeni Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani humo.