Imewekwa: 25 May, 2022
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini imepokea maombi ya kurejea nauli za Mabasi Yaendayo Haraka jijini Dar es Salaam kutoka kwa Wakala wa DART. Kwa mujibu wa Kifungu Na. 21 cha Sheria Sura Na. 413, Mamlaka inapaswa kukusanya maoni ya wadau kabla ya kufikia uamuzi kuhusu viwango vya nauli vinavyopendekezwa