Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara ya Uchukuzi

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini

Piga Bure : 0800110019/0800110020
LATRA Logo

Hotuba ya Waziri wa Uchukuzi Mheshimiwa Prof. Makame Mnyaa Mbarawa (Mb.), akiwasilisha Bungeni Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka wa Fedha 2024/25
Imewekwa: 06 May, 2024

Mheshimiwa Spika, utakumbuka kuwa, tarehe 30 Agosti, 2023 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan aliunda Wizara ya Uchukuzi baada ya kugawanywa kwa iliyokuwa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi. Tangu kuundwa kwake, Wizara ya Uchukuzi imeendelea kutekeleza kazi zake kulingana na Hati ya Mgawanyo wa Majukumu iliyotolewa. Kwa heshima kubwa, ninaomba nimshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuendelea kuniamini na kuniteua kuwa Waziri wa Uchukuzi. Ninaomba kumhakikishia Mhe. Rais na Bunge lako Tukufu kuwa nitaendelea kutekeleza majukumu yangu kwa uaminifu mkubwa ili  kuliletea Taifa letu maendeleo. Kwa muktadha huo, naomba kutoa Hotuba yangu ya kwanza ya Wizara ya Uchukuzi ambayo imejikita katika masuala ya usimamizi na uwezeshaji wa maendeleo ya miundombinu, huduma za uchukuzi na hali ya hewa kwa lengo la kuleta maendeleo endelevu kwa Wananchi. Aidha, napenda kumpongeza Mheshimiwa Innocent Lugha Bashungwa (Mb.) kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Ujenzi baada ya iliyokuwa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kugawanywa.

Soma zaidi

Mrejesho

Mrejesho, Malalamiko au Wazo