Imewekwa: 11 Oct, 2023
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) kwa kuzingatia changamoto ya usafiri katika barabara ya Morogoro na juhudi zinazofanywa na UDART kuboresha huduma za usafiri, Mamlaka imeamua kuchukua hatua za dharura kwa kuwakaribisha wasafirishaji kuomba leseni kwenye njia tajwa hapo chini ili kusaidia wananchi wanaopata adha ya usafiri wakati wa kuelekea kwenye majukumu ya kujenga uchumi wa Nchi yetu.