Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara ya Uchukuzi

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini

Piga Bure : 0800110019/0800110020
LATRA Logo

Kuomba Leseni za Usafiri wa Kukodi-Pikipiki za magurudumu mawili na matatu
Imewekwa: 12 May, 2023

Nyaraka zinazohitajika

Kadi ya usajili wa Pikipiki

 Hatua za Kufuata

a) Kupata linki ya mfumo,  ingia kwenye tovuti ya Mamlaka www.latra.go.tz, fungua huduma mtandao kisha chagua RRIMS. (Unaweza pia kupata linki ya mfumo moja kwa moja kwa kuandika www.rrims.latra.go.tz )

b) Itafunguka linki ya mfumo wa RRIMS, kisha ingiza baruapepe na nywila yako kwenye sehemu husika,

c) Chagua neno lililoandikwa Maombi ya leseni, bofya sehemu iliyoandikwa Bodaboda/ Bajaji

d) Chagua neno Ongeza gari

e) Jaza na hifadhi taarifa zinazohitajika, ambatisha nakala ya Kadi ya pikipiki kisha wasilisha maombi hayo kwenye ofisi ya LATRA uliyochagua

f) Maombi ya leseni yatashughulikiwa ndani ya saa ishirini na nne (24)

g) Msafirishaji utapata ankara ya Malipo (Control number)

h) Utalipia kupitia ankara ya malipo (Control number) kwa kutumia huduma za kifedha kwenye mitandao ya simu. (tigopesa, Mpesa,Airtel Money, Halopesa, T-pesa n.k)  benki na mawakala wa benki (NMB, NBC, Azania, nk)

i) Baada ya malipo unaweza kuchukua leseni katika ofisi ya Mamlaka iliyo karibu.

Zingatia

Hatua za maombi ya leseni, zitafuatwa na waombaji wa leseni wanaohuisha leseni, kubadili njia/huduma/ratiba baada ya mwombaji wa leseni  kuchagua huduma anayohitaji.

Uhai wa Leseni: Mwaka mmoja

Gharama za maombi ya leseni

Unapotuma maombi ya leseni gharama yake TZS. 2,000/= au Dola 5

Gharama za leseni

  • Leseni ya Pikipiki magurudumu mawili TZS. 15,000/= au Dola 20
  • Leseni ya Pikipiki magurudumu matatu TZS. 20,000/= au Dola 20

Zingatia

Malipo yote yafanyike kwa  ankara ya malipo (control number)/ namba ya kumbukumbu ya malipo iliyotolewa na Mamlaka.

Mrejesho

Mrejesho, Malalamiko au Wazo