Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara ya Uchukuzi

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini

Piga Bure : 0800110019/0800110020
LATRA Logo

Kusajiliwa na Kuthibitishwa (Wahudumu na Madereva wa Vyombo vya Moto Kibiashara)
Imewekwa: 12 May, 2023

1. Maombi ya Dereva Kusajiliwa

Nyaraka zinazohitajika

a) Leseni ya udereva,

b) Cheti cha taaluma ya udereva kutoka chuo kinachotambulika na  Serikali

Hatua za Kufuata

a) Kupata linki ya mfumo, kwenye tovuti www.latra.go.tz, fungua huduma mtandao kisha chagua RRIMS. (Unaweza pia kupata linki ya mfumo moja kwa moja kwa kuandika www.rrims.latra.go.tz )

b) Itafunguka linki ya mfumo wa RRIMS, kisha ingiza baruapepe na nywila yako kwenye sehemu husika,

c) Chagua neno lililoandikwa usajili wa Dereva au Kondakta,

d) Jaza na hifadhi  taarifa zinazohitajika, ambatisha nakala za nyaraka zinazohitajika kisha wasilisha maombi,

e) Maombi yatashughulikiwa ndani ya saa ishirini na nne (24) na mhudumu  atapata ankara ya Malipo (Control number),

f) Utalipia kupitia ankara ya malipo (Control number) kwa kutumia huduma za kifedha kwenye mitandao ya simu. (tigopesa, Mpesa,Airtel Money, Halopesa, T-pesa n.k)  benki na mawakala wa benki (NMB, NBC, Azania, nk)

Zingatia

Kwa dereva aliyesajiliwa kwenye mfumo na kulipa ada ya usajili, hatalipa ada ya kuthibitishwa pindi atakapowasilisha maombi ya kufanya mtihani.

Gharama

Ada ya usajili TZS.20,000/=

Zingatia

Malipo yote yafanyike kwa  ankara ya malipo (Control number)/ namba ya kumbukumbu ya malipo iliyotolewa na Mamlaka.

2) Maombi ya Dereva Kuthibitishwa

Nyaraka zinazohitajika

a) Leseni hai ya udereva,

b) Cheti cha taaluma ya udereva kutoka VETA au Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT),

c) Cheti cha uthibitisho wa afya kutoka kwenye hospitali inayotambulika na  Serikali

Hatua za Kufuata

a) Kupata linki ya mfumo, kwenye tovuti www.latra.go.tz, fungua huduma mtandao kisha chagua RRIMS. (Unaweza pia kupata linki ya mfumo moja kwa moja kwa kuandika www.rrims.latra.go.tz )

b) Itafunguka linki ya mfumo wa RRIMS, kisha ingiza baruapepe na nywila yako kwenye sehemu husika,

c) Chagua neno lililoandikwa usajili wa Dereva au Kondakta,

d) Jaza na hifadhi  taarifa zinazohitajika, ambatisha nakala za nyaraka zinazohitajika kisha wasilisha maombi.

e) Maombi yatashughulikiwa ndani ya saa ishirini na nne (24) na dereva  atapata ankara ya Malipo (Control number),

f) Utalipia kupitia ankara ya malipo (Control number) kwa kutumia huduma za kifedha kwenye mitandao ya simu. (tigopesa, Mpesa,Airtel Money, Halopesa, T-pesa n.k)  benki na mawakala wa benki (NMB, NBC, Azania, nk)

g) Dereva ataweka nafasi ya kufanya mtihani kwa kuchagua tarehe na muda,

h) Mtihani utasahihishwa na mfumo ( kidigitali),

i) Dereva atapata matokeo ya mtihani kwa njia ya ujumbe mfupi, saa moja baada ya kuwasilisha mtihani wake kwenye mfumo.

j) Dereva aliyefaulu mtihani atapatiwa Cheti baada ya taratibu zote kukamilika.

Zingatia

Hatua za maombi ya kuthibitishwa/kusajiliwa, zitafuatwa na waombaji wanaohuisha vyeti vya uthibitisho baada ya mwombaji kuchagua huduma anayohitaji.

Gharama

a) Ada ya maombi ya Cheti TZS. 10,000/=

b) Ada ya Cheti cha Dereva TZS.10,000/=

Uhai wa Cheti: Miaka miwili

Zingatia

Malipo yote yafanyike kwa  ankara ya malipo (Control number)/ namba ya kumbukumbu ya malipo iliyotolewa na Mamlaka.

3. Maombi ya Mhudumu Kusajiliwa

Nyaraka zinazohitajika

a) Cheti cha uthibitisho wa afya kutoka hospitali inayotambulika na  Serikali.

b) Cheti cha mafunzo ya huduma ya kwanza au huduma bora kwa wateja au mafunzo yoyote kwenye sekta ya usafirishaji

Hatua za Kufuata

a) Kupata linki ya mfumo, kwenye tovuti www.latra.go.tz, fungua huduma mtandao kisha chagua RRIMS. (Unaweza pia kupata linki ya mfumo moja kwa moja kwa kuandika www.rrims.latra.go.tz )

b) Itafunguka linki ya mfumo wa RRIMS, kisha ingiza baruapepe na nywila yako kwenye sehemu husika,

c) Chagua neno lililoandikwa usajili wa Dereva au mhudumu,

d) Jaza na hifadhi  taarifa zinazohitajika, ambatisha nakala za nyaraka zinazohitajika kisha wasilisha maombi,

e) Maombi yatashughulikiwa ndani ya saa ishirini na nne (24) na mhudumu  atapata ankara ya Malipo (Control number)

f) Utalipia kupitia ankara ya malipo (Control number) kwa kutumia huduma za kifedha kwenye mitandao ya simu. (tigopesa, Mpesa,Airtel Money, Halopesa, T-pesa n.k)  benki na mawakala wa benki (NMB, NBC, Azania, nk)

g) Mhudumu aliyekidhii vigezo atapatiwa kadi ya usajili.

Gharama

a) kusajiliwa TZS. 10,000/=

b) Ada ya kadi ya mhudumu (Crew) TZS.10,000/=

Zingatia

Malipo yote yafanyike kwa  ankara ya malipo (Control number)/ namba ya kumbukumbu ya malipo iliyotolewa na Mamlaka

Mrejesho

Mrejesho, Malalamiko au Wazo