Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara ya Uchukuzi

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini

Piga Bure : 0800110019/0800110020
LATRA Logo

Kuomba Leseni za Magari ya Mizigo
Imewekwa: 09 May, 2022

Nyaraka zinazohitajika

a) Kadi ya usajili wa gari;

b) Hati ya Bima iliyo hai;

c) Hati ya ukaguzi wa gari kutoka Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani pamoja na risiti yake ya malipo.

 Hatua za Kufuata

a) Kupata linki ya mfumo, ingia kwenye tovuti ya Mamlaka www.latra.go.tz, fungua huduma mtandao kisha chagua RRIMS. (Unaweza pia kupata linki ya mfumo moja kwa moja kwa kuandika www.rrims.latra.go.tz )

b) Itafunguka linki ya mfumo wa RRIMS, kisha ingiza baruapepe na nywila yako kwenye sehemu husika,

c) Chagua neno lililoandikwa Maombi ya leseni, bofya Maombi ya Leseni Magari ya Mizigo,

d) Chagua neno Ongeza gari,

e) Jaza na hifadhi taarifa zinazohitajika,  ambatisha nakala za vielelezo vinavyohitajika  kisha, wasilisha maombi hayo kwenye ofisi ya LATRA uliyochagua,

f) Maombi ya leseni yatashughulikiwa na Maafisa leseni ndani ya saa ishirini na nne (24),

g) Msafirishaji utapata ankara ya malipo (Control number)

h) Utalipia kupitia ankara ya malipo (Control number) kwa kutumia huduma za kifedha kwenye mitandao ya simu. (tigopesa, Mpesa, Airtel Money, Halopesa, T-pesa n.k)  benki na mawakala wa benki (NMB, NBC, Azania, nk)

i) Baada ya malipo unaweza kuchapa leseni yako mtandaoni kupitia akaunti yako RRIMS.

Zingatia

Hatua za maombi ya leseni, zitafuatwa na waombaji wa leseni wanaohuisha leseni baada ya mwombaji wa leseni  kuchagua huduma anayohitaji.

 

Uhai wa Leseni: Mwaka mmoja

Gharama

  • Unapotuma maombi ya leseni gharama yake ni TZS. 20,000/= au Dola 15
  • Gharama ya kubadili taarifa za mmiliki ni TZS. 30,000/= au Dola 10
  • Gharama ya kuvuka mpaka ni TZS. 200,000/= au Dola 50
  • Gari lenye uzito usiozidi tani moja TZS. 50,000/=
  • Gari lenye uzito tani 1 na usiozidi tani 5 TZS. 100,000/= au Dola 50
  • Gari linalozidi tani 5 na lisilozidi tani 10 TZS. 150,000/= au Dola 70
  • Gari linalozidi tani 10 na lisilozidi tani 20 TZS. 250,000/= au Dola 115
  • Gari linalozidi tani 20 na kuendelea TZS. 350,000/=  au Dola 165

Gharama

i)  Ada katika Dola italipwa sawia katika shilingi ya Kitanzania ya siku husika.

ii) Malipo yote yafanyike kwa  ankara ya malipo (Control number)/ namba ya kumbukumbu ya malipo iliyotolewa na Mamlaka

 

 

 

 

Mrejesho

Mrejesho, Malalamiko au Wazo