Imewekwa: 10 Oct, 2023
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua vyema umuhimu wa ulinzi na usalama wa miuondombinu ya reli. Serikali imeendelea kujenga miundombinu mipya ya reli na kuboresha iliyopo ili uendeshaji wa shughuli za reli uwe na tija. Usalama wa reli ndiyo kichocheo kikubwa cha uchumi wetu hapa Nchini, na eneo zima la Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Afrika kwa jumla.