Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara ya Uchukuzi

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini

Piga Bure : 0800110019/0800110020
LATRA Logo

Hotuba ya Mhe. Prof. Makame M. Mbarawa (Mb), Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi kwenye Hafla ya Uzinduzi wa Bodi ya Wakurugenzi ya LATRA, Jumanne, Tarehe 11 Julai, 2023 
Imewekwa: 11 Jul, 2023

Awali ya yote, nianze kwa kumshururu Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema, kwa kutujalia uhai, afya njema na fursa ya kukutana hapa kwa lengo la kuzindua Bodi ya Pili ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA).  Niwashukuru Mwenyekiti wa Bodi na Mkurugenzi Mkuu LATRA kwa kunialika katika shughuli hii ya kuzindua Bodi ya LATRA.

 

Napenda kutumia fursa huu kumshukuru na kumpongeza sana Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa uongozi wake mahiri na ufuatiliaji wake wa karibu wa utendaji kazi wa Wizara na utendaji wa Taasisi za Serikali ili ziweze kutimiza vyema majukumu yake.

 

Ndugu Mwenyekiti na Wajumbe wa Bodi;

Leo tumekusanyika hapa kwa ajili ya hafla ya uzinduzi wa bodi ya pili ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA). Nitumie fursa hii kukupongeza Prof. Ahmed Mohammed Ame, kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Pili ya Wakurugenzi ya LATRA. Pia, ninawapongeza Wajumbe wote sita (6) wa Bodi hii mlioaminiwa na kuteuliwa.

 

Ndugu Mwenyekiti na Wajumbe wa Bodi;

Napenda mfahamu kwamba Mheshimiwa Rais aliamua kumteua Mwenyekiti mpya wa Bodi ya LATRA kutokana na sababu za kiafya za Dkt. John Ndunguru, aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi hii. Naomba kutumia fursa hii kumshukuru na kumpongeza Dkt. Ndunguru kwa mchango wake katika kuiongoza Bodi ya kwanza ya LATRA. Aidha, niwashukuru na kuwapongeza Wajumbe wa Bodi iliyopita kwa mazuri waliyoyatekeleza katika kipindi chenu.

Pakua hotuba

Mrejesho

Mrejesho, Malalamiko au Wazo