Bw. Abdallah Mitawi, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi ameiagiza Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji wa huduma za taksi mtandao nchini, ikiwemo kufanya ukaguzi wa mifumo hiyo na kuhakikisha taarifa zinazowasilishwa ni sahihi, kamili na zinapatikana kwa wakati.
Bw. Mitawi ametoa maelekezo hayo akimuwakilisha Mhe. Prof. Makame Mbarawa (Mb), Waziri wa Uchukuzi, katika Mkutano Mkuu wa kwanza wa Chama cha Madereva wa Taksi Mtandao Tanzania (TODA) uliofanyika Septemba 15, 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Karimjee, Dar es Salaam, ukiwa na lengo la kujadili maandalizi ya usafirishaji wa wageni kuelekea Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 pamoja na maendeleo ya huduma za taksi mtandao nchini.
Soma hapa hotuba ya Mhe. Prof. Makame Mbarawa (Mb), Waziri wa Uchukuzi,

