Imewekwa: 10 Dec, 2022
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) ilipokea maombi ya viwango vya nauli vinavyopendekezwa na Shirika la Reli Tanzania (TRC) kuhusu nauli za treni za abiria kwa njia za Reli ya Kisasa – ‘Standard Gauge Railway’ (SGR) kwa ajili ya huduma ya usafiri wa treni za abiria zinazotarajia kuanza kutoa huduma mwakani 2023.
Kwa mujibu wa Kifungu Na. 21 cha Sheria Na. 3 ya LATRA, 2019 Mamlaka inapaswa kukusanya maoni ya wadau kabla ya kufikia uamuzi wa kuridhia viwango vya nauli kwa huduma zinazodhibitiwa na Mamlaka ikiwemo nauli za treni.